Saturday, September 21, 2013

WATU WATATU WA FAMILIA MOJA WAUAWA KWA KUNYONGWA NA KUCHINJWA HUKO BUHONGWA JIJINI MWANZA...!!



Akiongea  na  ITV, mkuu wa  upelelezi  wa  makosa  ya  jinai  RCO Joseph  Konyo  amesema  kuwa  baba  wa  familia  hiyo  aliyejulikana  kwa  jina  la  Jonas  Lulinga  anaekadiriwa  kuwa  na  umri  wa  miaka  44  ameuawa  kwa  kuchinjwa  na  kisu  huku  mkewe  na  mtoto  wao  mchanga  wakiuawa  kwa  kunyongwa  na  waya  wa  umeme...
Tukio  hilo  linadaiwa  kutekelezwa  majira  ya  saa  nane  usiku  na  mtu  mmoja  ambaye  walimkaribisha  na  kuishi  nae  kwa  siku  nne....
Binti  mmoja  aliyesalimika  anasimulia  tukio  hilo  kwa  kina  katika  video  iliyopachikwa  hapo  chini.