Showing posts with label Rose ndauka. Show all posts
Showing posts with label Rose ndauka. Show all posts

Sunday, August 25, 2013

HUYU NDO BABA YAKE ROSE NDAUKA

Mr. Donatus Ndauka

Monday, August 12, 2013

ROSE NDAUKA AANZA KUPETA ANGA ZA MUZIKI.

MSANII wa filamu nchini Rose Ndauka kwa mara ya kwanza amefanya shoo ya aina yake ya nyimbo ya bongo fleva aliyoshirikiswa na kundi la TNG, katika tamasha la sikukuu ya Iddi lililofanyika Dar Live jijini Dar es Salaam. 
Msanii huyo sasa ameamua kufanya muziki ambapo ameweza kushirikishwa single inayoenda kwa jina la  'Crazy Love ' na kundi hilo ambapo siku hiyo ilikuwa maalumu kwake kwa ajili ya kutambulisha nyimbo hiyo. 
Akizungumza na mwaandishi wa habari hii baada ya kumaliza kufanya shoo hiyo, Rose aliweka wazi kuwa kuimba 'live' jukwaani kunatofauti na kazi ya filamu ambayo ameizoea. 
Alisema upande wa filamu ni rahisi kurekebisha makosa endapo ukihisi kukosea tofauti na kuimba live jukwaani kwani ukikosea hauwezi kupata nafasi ya kurekebisha hivyo umakini unahitajika katika kazi hiyo. 
"Mimi ni msanii na kuimba ni kipaji changu kingine, lakini kwenye uimbaji inahitajika umakini zaidi tofauti na nilikokuzoea" alisema Ndauka. 
Aliongezea kuwa anamshukuru mtayarishaji wa muziki P Funk kwa kuweza kutambua kipaji chake hicho cha uimbaji na kuweza kumpa nafasi ya kushiriki katika nyimbo hiyo. 
Kundi la hilo linaundwa na wasanii wawili akiwemo Chiwaman pamoja na 'Latino Man', ambapo wameachia single yao ikiambata na uzinduzi .

"JAPO NILITUHUMIWA KUGAWA PENZI GESTI, LAKINI NIMEPIMA NA SINA UKIMWI.... NANI MJANJA??"...ROSE NDAUKA


Baada  ya  kukabiliwa  na  skendo  ya  kugawa  uroda  kwa  msanii  Nasry  ndani  ya  Gesti, Rose  ndauka  ameamua  kukimbilia  hospitalini  ili  kuchukua  vipimo  vya  gonjwa  hatari  la  Ukimwi.....


Kupitia  ukurasa  wake  wa  mtandao  mmoja  wa  kijamii, Ndauka  aliposti  picha  ya  majibu  ya  vipimo    vya  UKIMWI   vilivyochukuliwa  katika  hospitali  ya   TMJ iliyopo  jijini  Dar es salaam....



Majibu  ya  vipimo  hivyo  yalionesha  kuwa  Rose  Ndauka  yuko  NEGATIVE.


Baada  ya  picha  hiyo, comment  kibao  zilianza  kumiminika  toka  kwa  mashabiki  wake.Wapo  waliompongeza  na  wapo  waliomponda.....


Waliomponda  walihoji  ni  kwa  nini  kawahi  kupima  na  kuyaanika  majibu  mtandaoni  wakati  MIEZI  MITATU  TANGU  ATUHUMIWE  HAIJAISHA??????.


Kwa  kawaida, hawa  wadudu  huonekana  katika  mzunguko  wa  damu  baada  ya  siku  90  tangu  ufanye  tendo  la  ndoa.