Showing posts with label irene uwoya. Show all posts
Showing posts with label irene uwoya. Show all posts

Saturday, August 16, 2014

JOHARI AMPA MAKAVU IRENE UWOYA KUWA NA TABIA YA KUJIACHIA NA KUPOTEZA MVUTO


Johari Blandina Chagula ambaye ni star mkongwe Swahiliwood amesema kuwa anamshukuru Mungu kwa kuutunza muonekanio wake na kuwa kama kijana licha ya umri wake kuwa mkubwa tofauti na baadhi ya waigizaji wenzake wa kike ambao hujiachia na kuonekana wazee licha ya umri wao kuwa mdogo.
Akizungumza na Filamucentral Johari alisema "Wasanii wa kike wengi ni watoto wadogo lakini kwa sababu ya kujiachia wanaonekana kama watu wazima lakini ukweli ni watoto wadogo sana, namshukru Mungu nimeanza sanaa kitambo lakini mwili wangu upo fiti,



Johari alimtolea mfano Irene Uwoya ambaye ni shoga'ke wa karibu kuwa anaonekana mkubwa kwasasa sababu ya kujiachia licha ya kwamba amempita miaka kadhaa. Vile vile Johari amesema kuwa kawasasa amerudi kwa moto wa kasi kama muigizaji kama awali baada ya kuwa upande wa producer kuwapa nafasi chipukizi ambao wengi amesema wameshindwa so amerudi mwenyewe kwenye game
CREDIT:SWAHILI WORLD

Monday, December 9, 2013

Hii ndio kauli ya Irene uwoya ya kufunga mwaka huu wa 2013. Inakuhusu na wewe

Hii ndio kauli ya Irene uwoya ya kufunga mwaka huu wa 2013. Inakuhusu na wewe
“Napenda kuchukua nafasii hiii kuomba samahan kwa wote nilio wakosea...napia mim nimewasamehe...nataka nimaliza mwaka kwa amani na upendo...nawapenda wote sina kinyongo na mtu...asante mwenyez mungu kwakunipa nguvu

Tuesday, November 12, 2013

IRENE UWOYA AANZA MAZOEZI YA KUPUNGUZA UZITO BAADA YA KUDAIWA KAJIACHIA SANA NA KUPOTEZA MVUTO WAKE.

Irene Uwoya ameamua kuanza mazoezi ya kupunguza unene na kujiweka fiti na kurudisha mvuto wake wa awali ambao unadaiwa kupotea mara baada ya kujifungua huku media na wataalamu wa fashion wakimuandama mara kwa mara kuwa kapoteza mvuto wa mwanzo kwa kujiachia kunenepeana kiasi cha kupoteza mvuto. Owoya yupo chini ya mwalimu wake wa mazoezi Rashid Matumla ambaye ni bondia maarufu nchini na pia wanakuja na filamu wakiwa pamoja ambayo inaitwa Raundi Ya 8.
akizungumza na Filamucentral "Nimejipanga kwa kufanya mazoezi ya nguvu chini ya mwalimu wangu Rashid Matumla na nipo fiti kwa ajili ya kujifua najua kuigiza ndio ajira yangu lakini nikijiachia na kunenepa bila mpango nitaanza kucheza nafasi za akina bibi muda si mrefu na najiona mwili
unavyoninyemelea sitaki manyama uzembe"

 Filamu hiyo imeshutiwa Tanga, Dar es salaam na Morogoro huku waigizaji wengine wakiwa ni Francis Cheka na Lumolwe Matovolwa.

Uwoya akiwa na Rashid Matumla....................

Friday, October 25, 2013

BATULI AFUNGUKA BAADA YA MADAI KUWA IRENE UWOYA ANAMUENDEA KWA WAGANGA ILI AMPOTEZE KWENYE FILAMU.


 

Siku za Hivi karibuni kumekuwa na tetesi zisizo rasmi kuwa mastaa wawili wa filamu Swahiliwood Yobnesh Yusuph(Batuli) na Irene Uwoya hawana maelewano mazuri chanzo kikidaiwa ni Irene Uwoya kutaka kumpoteza Batuli kwenye tasnia ya filamu ili asifurukute. Habari hizo zinaenda mbali zaidi zikidai kuwa kuna kipindi Batuli alikuwa anaumwa maeneo ya kifuani lakini baadhi ya watu wakiwemo wasanii wenzake wakiamini Uwoya ndiye kamfanyia mambo ya kilozi(ushirikina).
 Tetesi hizo tulizipuuza mwanzoni lakini zinaonekana kurudi tena kwa kasi hivyo Swahiliworldplanet iliamua kuwatafuta mastaa hao wawili ili watoe ufafanuzi wao wenyewe na wa kwanza kuulizwa alikuwa Uwoya hata hivyo namba yake ilionekana kutokuwa hewani alipotafutwa juzi na jana alipotumiwa ujumbe namba yake ilionekana bado haipo hewani. Batuli nae alitumiwa ujumbe juzi kuhusu issue hiyo lakini hakujibu mpaka jana usiku ndiyo alijibu akisema alikuwa busy sana. Batuli alisema "sina ubaya na msanii yeyote na moyo wangu ni mweupe na nina mapenzi na wasanii wenzangu wote, nawapenda sana anayeniwinda kwa ubaya Mungu atanipa ulinzi wake, sipendi uadui na mtu namuachia Mungu atanilipia yote"
Hata hivyo bado SWP inamsaka Uwoya kwa namba yake nyingine ili atoe ufafanuzi wake kuhusu issue hiyo na pindi akitoa maelezo yake basi utayasoma hapa hapa SWP.