Showing posts with label unyama. Show all posts
Showing posts with label unyama. Show all posts

Tuesday, September 23, 2014

WACHUNGAJI ARUSHA MBARONI KWA ULAWITI WA WATOTO KANISANI

WATOTO sita, wakiwemo wawili wa kiume wenye umri wa miaka 8 hadi 14 wameharibiwa vibaya sehemu zao za siri baada ya kubakwa kanisani na watu wanaodaiwa ni wachungaji.
Watoto sita waliobakwa kanisani na watu wanaodaiwa ni wachungaji.
Wakiwa katika Hospitali ya Mkoa wa Arusha, Mount Meru walikopelekwa kwa matibabu na kuangaliwa maambukizi ya magonjwa ya zinaa, watoto hao walidai kufanyiwa mchezo huo kwa nyakati tofauti  na wachungaji watatu wa kanisa hilo lililopo eneo la  Feed Force, Kwamorombo jijini Arusha.
Mmoja wa watoto hao anayesoma darasa la 4 katika shule ya msingi alieleza kuwa yeye na wenzake wamekuwa wakifanyiwa mchezo mchafu katika kanisa hilo baada ya wachungaji hao kuwapatia shilingi 2,000 za kufungia mdomo.
“Siku moja nilipofika shuleni wenzangu wakaniambia niende pale kanisani tukapewe hela, nilipofika niliwaona wenzangu wengine wakifanyiwa mchezo mchafu na mimi mchungaji aliniambia niiname akanifanyia kitendo kibaya na kunipa shilingi 2,000, niliumia sana,’’ alisema mwanafunzi mmoja.
Mwanafunzi mwingine alisema amekuwa akitoroka shuleni na wenzake na kwenda kwa watumishi hao ambapo huwaingiza katika kanisa hilo na kujifanya wanawaombea baadaye huwafanyia mchezo mbaya.
Mbunge wa Arusha Mjini kwa tiketi ya Chadema, Godbless Lema.
“Tukifika huwa wanatufungia ndani na kutuambia tuwanyonye, baadaye wanatubaka  na wakimaliza wanatuambia tukisema kwa mtu yeyote watatuchinja na kutuzika ndani ya kanisa lao,” alisema denti huyo.
Wanafunzi hao walieleza kuwa watumishi hao huwarubuni kwa kuwaeleza kuwa watawasaidia kuwasomesha iwapo watakuwa wakienda kwenye kanisa hilo na kuwaingilia.
Mzazi mmoja wa watoto hao, Julius, mkazi wa Kwamorombo alisema mtoto wake alimweleza kwamba amekuwa akifanyiwa mchezo mbaya na watumishi hao baada ya kupewa shilingi 2,000.
Alisema aligundua hilo kufuatia tabia ya mtoto wake kuchelewa kurudi nyumbani.
Naye Mbunge wa Arusha Mjini kwa tiketi ya Chadema, Godbless Lema ambaye alifika hospitalini kuwajulia hali watoto hao alisikitishwa na kitendo hicho na kulitaka jeshi la polisi lifanye uchunguzi wa kina kwa kushirikiana na vipimo vya kidaktari ili kupata ukweli wa tukio hilo.
“Nimeongea na mkuu wa mkoa, Magesa Mulongo ambaye ameahidi kulifuatilia kwa kina suala hili na kujua undani wake,’’ alisema Lema.
Kamanda wa Polisi Arusha, Leberatus Sabas.
Hata hivyo, watoto hao baadaye walihamishiwa katika Hospitali ya Seliani kwa ajili ya vipimo zaidi huku taarifa za awali zikithibitishwa na daktari wa hospitali hiyo kuwa, baadhi yao walikutwa na michubuko na kupanuka sehemu za siri hali inayooneshwa kuingiliwa.
Watuhumiwa wa tukio hilo wanashikiliwa katika Kituo Kikuu cha Polisi jijini hapa  kwa uchunguzi zaidi na Kamanda wa Polisi Arusha, Leberatus Sabas amethibitisha kutokea kwa tukio hilo

CREDIT:GPL

Tuesday, July 8, 2014

ARUSHA TENA....! WATU NANE WANADAIWA KUJERUHIWA VIBAYA NA BOMU NDANI YA MGAHAWA


  Pichani ni Askari wa Jeshi la Wananchi JWTZ kitengo cha Mabomu wakiwa katika eneo la tukio ambapo bomu lilirushwa ndani ya Mgahawa ujulikanao kwa jina la Traditional Indian Cusine uliopo pembeni ya hotel ya Gymkana jijini Arusha,aidha taarifa za awali zinaeleza kuwa watu nane wamejeruhiwa vibaya na mlipuko huo .
 Picha ni majeruhi wa mlipuko wa Bomu uliotokea katika mgahawa wa Traditional Indian Cusine aliyejulikana kwa jina la Deepak Gupta (25),akiwa amelazwa katika hospitali ya Selian,katika chumba cha watu mahututi (ICU),mara baada ya kukatwa mguu wake mmoja wa kushoto kutokana na mhuu huo kujeruhiwa vibaya na bomu.
 Sehemu ya baadhi ya watu waliojeruhiwa kwenye mlipuko wa bomu uliotokea jana usiku katika mgahawa wa Traditional Indian Cusine wakiwa wamelazwa katika hospitali ya Selian,jijini Arusha kwa matibabu. 

Monday, July 7, 2014

Wasichana 63 waliotekwa na Boko Haram watoroka na kurejea Nyumbani

WAPIGANAJI WA BOKO HARAM TAARIFA KUTOKA KASKAZINI MASHARIKI MWA NIGERIA ZINASEMA KUWA ZAIDI YA WANAWAKE 60 WAKIWEMO WASICHANA WA UMRI MDOGO WALIOTEKWA NYARA MWEZI JANA NA BOKO HARAM WAMEKWEPA.TAARIFA HII INAKUJA WAKATI SAWA NA TAARIFA ZA KUTOKEA MAKABILIANO MAKALI KATI YA JESHI LA NIGERIA NA WAPIGANAJI WA KUNDI HILO.


Serikali ya Nigeria imeitisha uchunguzi wa kina juu ya namna walivyotoweka wasichana hao.Wanawake hao wanaaminiwa kuwa miongoni mwa wanawake 68 waliotekwa nyara mwezi uliopita karibu na mji wa Damboa Kaskazni Mashariki mwa jimbo la Borno.Hali ya usama ni mbaya sana huku miundo mbinu duni ikichangia kuifanya hali ngumu kuweza kufikia maficho ya kundi hilo na pia kubaini idadi ya wasichana waliotoroka kutoka mikononi mwa Boko Haram.


BBC imeongea na jamaa ya wasichana watatu ambao walitoroka. Sasa wako salama nyumbani kwao na mmoja wao amesema kwamba wasichana wengi wamefanikiwa kutoroka. 
Baadhi ya vyombo vya habari nchini humo vinadai kuwa huenda wasichana hao walitoroka siku ya Ijumaa, pale watekaji nyara walipokwenda kushamblia kambi ya kijeshi.

Maafisa wakuu hata hivyo bado hawajaweza kuthibitisha kukwepa kwa wasichana hao.
Wakati huohuo hapajakuwa na taarifa zozote kuhusu wasichana 200 waliotekwa nyara katika shule ye mabweni ya Chibok mwezi Aprili.

Hatua ambayo imekemewa vikali na jamii ya kimataifa huku baadhi ya mataifa kama vile Marekani, Uingereza na hata Ufaransa wakijitolea kuisaidia serikali ya Nigeria kuwasaka wasichana hao.

CHANZO: bbc

Sunday, July 6, 2014

HUYU NDIYE SHEIKH ALIYELIPULIWA KWA BOMU ARUSHA

Sheikh wa Msikiti wa Qiblatan, Sood Ally Sood (37), uliopo Kilombero jijini Arusha amelipuliwa na bomu la kurusha kwa mkono akiwa nyumbani kwake wakati wakila daku hapa akiwa amelazwa katika Hospitali ya Mt. Meru, alijeruhiwa miguuni na mapajani.
Shekhe Muhaji Hussein Kifea alijeruhiwa miguu na mapajani akiwa kitandani baada ya kutibiwa.
Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Magessa Mulongo akiwajulia hali majeruhi.
Kamanda wa Polisi wa mkoa wa Arusha, SACP Liberatus Sabas akiwajulia hali mashekhe hao.
 

Sheikh wa Msikiti wa Qiblatan,Sood Ally Sood (37) uliopo Kilombero jijini hapa amejeruhiwa kwa bomu la kurushwa kwa mkono alipokuwa akila daku nyumbani usiku wa kuamkia jana.
Pamoja na Sheikh Sood, mtu mwingine aliyekuwa nyumbani kwake,aliyetajwa kwa jina la Muhaji Kifea (38) mkazi wa Sinza jijini Dar es Salaam pia amejeruhiwa katika tukio hilo na wote wamelazwa katika Hospitali ya Mkoa ya Mount Meru kwa matibabu.



Sheikh alijeruhiwa miguu yake yote na mapajani huku Kifea akipata majeraha makubwa miguuni na kupoteza baadhi ya vidole vya miguu yote.



Akizungumza hospitalini hapo, Sheikh, Sood alisema tukio hilo lilitokea nyumbani kwake eneo la Majengo ya chini, usiku wa kuamkia jana saa 5:00 wakati yeye pamoja na mgeni wake walikuwa wakila chakula sebuleni.



“Nikiwa sijui hili wala lile nilishtushwa na mlipuko ulioambatana na vyuma mbalimbali vilivyokuwa vikiruka hewani ambapo bomu hilo linaelezwa kuwa ni guruneti lililorushwa kupitia dirishani baada ya watu wasiofahamika kufanikiwa kuvunja kioo cha dirisha la chumba tulichokuwamo,” alisema Sheikh Sood.



Alidai anawajua waliotekeleza shambulio hilo kwa sababu amekuwa akipokea vitisho kutoka kwa watu anaowafahamu na tayari alikuwa ametoa taarifa kwa vyombo vya dola.



Alisema kuwa siku tatu kabla ya tukio hilo alikoswakoswa kupigwa risasi na watu wasiofahamika wakati akitoka msikitini na akatoa taarifa Kituo Kikuu cha Polisi jijini Arusha kuhusu tukio hilo. Sood anasema kuna baadhi ya vijana anawatuhumu juu ya matukio hayo.



Sheikh huyo ambaye ni Kiongozi wa dhehebu la Answar sun Kanda ya Kaskazini amekuwa akitofautiana na waumini wenzake kutokana na msimamo wake wa kutokukubaliana na baadhi ya waumini wenye msimamo mkali wa msikiti huo.



Mkuu wa Mkoa wa Arusha,  Magesa Mulongo alikemea matukio ya mabomu yanayolitikisa Jiji la Arusha katika siku za karibuni na kuviagiza vyombo dola kufanya uchunguzi wa kina kubaini wahusika wote ili hatua za kisheria zichukuliwe dhidi yao.



“Uchunguzi wa awali unaonyesha tukio hili limetekelezwa na watu walio karibu na Sheikh. Polisi wanaendelea na uchunguzi kwa sababu baadhi ya watu wanaotajwa kuhusika kwenye tukio hili pia ni miongoni mwa watuhumiwa kwenye matukio mengine ya milipuko ya bomu Arusha,” alisema Mulongo.



Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha, Liberatusi Sabasi alithibitisha kutokea kwa tukio hilo na kueleza kuwa majeruhi wanaendelea vyema huku polisi wakiendelea na uchunguzi wa kina kuwabaini wahusika.



Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema alielezea kusikitishwa na matukio ya milipuko ya mabomu Arusha na kuliomba jeshi la polisi kufanya uchunguzi wa kina kuwakamata wahusika bila kujali vyeo, nyadhifa, dini, itikadi wala rangi zao.



“Arusha tunapita katika kipindi kigumu sana. Kwanza tulishuhudia mlipuko wa bomu kanisani, ikafuatiwa na lile la mkutano wa hadhara wa Chadema, kabla ya mwingine kulipuka kwenye baa na sasa nyumbani kwa Sheikh,” alisema Lema.

Saturday, July 5, 2014

yule Mfungwa askari wa jkt aliyemuua mtoto wa Fundikira afariki dunia





                                               Mfungwa Sajini Rhoda Robert

Mfungwa Sajini Rhoda Robert aliyekuwa anasubiri adhabu ya kunyongwa kwa kosa la kumuua mtoto wa kigogo Swetu Fundikira, amefariki dunia wakati akitibiwa katika hospitali ya mkoa ya Dodoma, kufuatia hali yake kubadilika kutokana na kuishiwa damu mwilini.

Rhoda aliyekuwa askari wa kikosi cha Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) Mbweni na wenzake Koplo Ally Ngumbe na Mohamed Rashid, walihukumiwa kunyongwa hadi kufa na Mahakama Kuu kanda ya Dar es Salaam, baada ya kupatikana na hatia ya kumuua mtoto wa Chifu Abdallah Fundikira.
Hukumu hiyo ilitolewa na Jaji Zainabu Muruke Novemba 20, 2012.

Hadi mauti yanamkuta, Jaji Muruke aliyesikiliza na kutoa hukumu ya kesi hiyo alikuwa hajasaini hukumu hiyo na kuwafanya wafungwa hao kushindwa kukata rufaa Mahakama ya Rufani kupinga hukumu hiyo.

Mapema mwaka huu wakili wa wafungwa hao, Kaloli Muruge, aliiambia NIPASHE kuwa aliwasilisha kusudio la kukata rufaa lakini kikwazo ilikuwa ni nakala ya hukumu ambayo jaji alikuwa hajaisaini.

Habari za kuaminika kutoka Gereza la Isanga mkoani Dodoma ambapo mfungwa huyo alikuwa akisubiri kunyongwa, zilisema kuwa Sajenti Rhoda alikuwa amelazwa katika hospitali hiyo akisumbuliwa na maradhi.

Alisema hali ya mfungwa huyo ilibadilika na kufariki dunia akiwa hospitalini hapo.





“Alizikwa gerezani kwa sababu alikuwa ni mfungwa ambaye kisheria hairuhusiwi kuzikwa uraiani lakini mwishoni mwa wiki ndugu zake waliarifiwa kuhusu kifo chake kabla ya mazishi na walifika na kuonyeshwa kaburi lilipo,” kilieleza chanzo chetu cha habari.

NIPASHE ilizungumza na  Mkuu wa Gereza la Isanga, Makoti Mwaibale, ambaye alithibitisha kufariki kwa mfungwa huyo. Alisema mfungwa huyo alifariki dunia Juni 20, mwaka huu katika hospitali hiyo akiwa anapatiwa matibabu.

Alisema Rhoda aliumwa na kupelekwa hospitalini  Juni 15,  mwaka huu ambapo alilazwa huku akiendelea na matibabu kwani ugonjwa uliokuwa unamkabili ulimsababishia kupungua kwa damu.

"Ugonjwa wa mtu ni siri hivyo alikuwa akiongezewa damu na ilipofika Juni 20 majira ya saa 1 asubuhi alifariki dunia," alisema. Mwaibale alisema mfungwa huyo alizikwa siku hiyo katika makaburi ya wafungwa yaliyopo Dodoma.

Alisema mume wa marehemu pamoja na mjomba wake walitaka kuuchukua mwili huo kwa ajili ya mazishi lakini haikuwezekana kwa mujibu wa sheria.
Hata hivyo, alisema kwa mfungwa ambaye amehukumiwa kunyongwa hadi kufa akifariki anazikwa na magereza lakini angekuwa ni mahabusu wa kawaida mwili huo ungekabidhiwa kwa ndugu zake.

Alisema ndugu wa marehemu hawakushirikishwa katika mazishi kwa kuwa kuna sheria zinazowaongoza katika jambo hilo.Mwaibale alisema ndugu zake akiwamo mume wake walifika Juni 22, na kuonyeshwa kaburi la mfungwa huyo lilipo.

Hukumu ya askari hao ilisomwa na Jaji Muruke alisema ingawa hakuna ushahidi wa moja kwa moja kuwa washtakiwa hao ndiyo waliomuua Fundikira, ushahidi uliotolewa na  upande wa mashtaka (Jamhuri) ulikuwa ni ushahidi wa mazingira, kwamba Jamhuri imeweza kuthibitisha mashtaka hayo.

Alisema kuwa anakubaliana na mtiririko wa ushahidi wa upande wa mashtaka kama ulivyoelezwa na mashahidi wake sita akiwemo daktari aliyeufanyia uchunguzi mwili wa marehemu pamoja na  askari polisi wawili ambao washtakiwa katika utetezi wao walishindwa kuuvunja.

“Sheria iko wazi ukiondoka na mtu au ukionekana naye kwa mara ya mwisho na baadaye mtu huyo akapatikana na madhara, wewe ndiyo unawajibika kutoa maelezo ya kina kuhusu yaliyompata mtu huyo,” alisema Jaji Muruke na kuongeza;

“Kisheria ukitoa maelezo ambayo hayajakidhi haja na yana utata ni faida kwa upande wa mashtaka ambao hutegemea ushahidi wa mazingira. Maelezo ya kina hayajatolewa na washtakiwa wote.”

Aliendelea,  “Ushahidi wa Jamhuri japokuwa ni wa mazingira, umejengwa thabiti na upande wa utetezi haukuweza kujenga matundu, ama kuuvunja mnyororo huo,  kidole kinawaelekea wao.”

Jaji Muruke alisisitiza kuwa katika kesi hiyo licha ya kuwa kuna ushahidi wa kimazingira, upande wa mashtaka umeweza kuthibitisha mashtaka.







                                             marehemu fundikira

Sajini Roda na Koplo Mohamed Rashid wote wa JKT Mbweni na Koplo Ally Ngumbe (37) wa Kikosi cha JWTZ Kunduchi, walimpiga Fundikira, Januari 23 mwaka huu  saa 7:30 usiku wilayani Kinondoni jijini Dar es Salaam na baadaye kufariki dunia usiku huohuo wa kuamkia Januari 24, mwaka 2010, katika Hospitali ya Taifa Muhimbili.

 
CHANZO: NIPASHE

Thursday, May 15, 2014

BAADA YA ALBINO KUTENDEWA UNYAMA SIMIYU, SERIKALI IMEOMBWA WAGANGA WA KIENYEJI WAFUTIWE VIBALI

Polisi nchini Tanzania wamewakamata waganga wawili wa kienyeji baada ya mwanamke mmoja mwenye ulemavu wa ngozi au Abino kuuwawa kwa kuchinjwa.
Moja ya miguu yake pamoja na vidole vilinyofolewa baada ya shambulizi hilo la hapo jana Jumanne katika mkoa wa Simiyu Kaskazini Mashariki mwa Tanzania. Kumekuwa na visa vingi vya mauaji ya albino katika eneo hilo hapo awali.Shirika la kutetea haki za watu wenye ulemavu wa ngozi Albino la 'Under the Same Sun limeiomba serikali ya nchi hiyo kufuta vibali na shughuli zote za waganga wa jadi kwa madai kuwa wao ndiyo chanzo cha kuuawa kwao.
Kuuawa kwa mwanamke Munghu Lugata mlemavu wa ngozi toka kijiji cha Gasuma mkoani Simiyu Kaskazini Magharibi mwa nchi hiyo kumeacha hisia na uchungu kwa walemavu wengine waliopata mikasa hiyo.
Akizungumza na mwandishi wa BBC Leonrad Mubali kwa uchungu na kilio, Mariamu Staford mlemavu wa ngozi Albino amesema kwamba tukio la kuuawa kwa Munghu Lugata mwanamke mwenye umri wa miaka 40 juzi linamkumbusha mkasa wake uliomkuta wa kukatwa mikono yake yote, zaidi ya miaka mitano iliyopita na sasa anatumia mikono ya bandia ya vyuma huku akisema malengo yake mengi yamekwama.
Albino wamekuwa wakihangaishwa sana nchini Tanzania ambako baadhi ya watu wanaamini kuwa dawa za miujiza zinazotengezwa kutokana na viungo vya miili yao zinaleta bahati nzuri.
Mashambulizi yamepungua katika siku za hivi karibuni lakini mauaji ya hivi punde yamepelekea shirika moja la kutetea haki za Albino kutoa wito kwa serikali kupiga marufuku waganga wote wa kienyeji.
Matukio mengi ya maujia ya walemavu nchini Tanzania yamekuwa yakihusishwa na imani za kishirikina huku waganga wa jadi wakihusishwa.
Mkoa wa Simiyu ni moja katika maeneo kaskazini magharibi mwa Tanzania yenye matukio mengi ya mauaji hayo.
Hivi karibuni nchini Tanzania umezinduliwa mnara maalumu unaoitwa NITHAMINI, mnara pekee duniani unaowakilisha kupinga mauaji ya albino huku Tanzania ikiwa ni moja ya nchi yenye matukio mengi ya ukatili dhidi ya walemavu hao

Monday, November 25, 2013

Watoto watekwa , walawitiwa na kuteswa kinyama ndani ya handaki lilipo katika msitu wa Mabwepande


 

Zaidi ya watoto 60 wanadaiwa kutekwa na kufichwa katika handaki lililopo kwenye msitu wa Mabwepande, Wilaya ya Kinondoni ,Dar es Salaam, ambalo ndani yake kuna jengo kubwa lenye vyumba.

Utekaji huo unadaiwa kufanywa na raia wa kigeni (Wazungu), wakishirikiana na Watanzania ambapo watoto hao hufungiwa katika vyumba hivyo, kuteswa, kulawitiwa na kubakwa.

Mtoto Emmanuel Robert (11) anayesoma darasa la tano Shule ya Msingi Maendeleo iliyopo Tabata, Segerea, Dar es Salaam na mdogo wake Godianus Robert (8), anayesoma darasa la tatu shuleni hapo, ndio waliofichua ukatili huo mwishoni mwa wiki.

Watoto hao walitekwa na Wazungu w awiliasubuhiyaSeptemba2mwaka huu, wak ati wakiendas huleni n akufan ikiwa kutoroka katikaj engohiloSeptemba 23 mwaka huu.

Wakiwa wamechoka na afya zao kuzorota katika Kituo kidogo cha Polisi, Kibaha Maili Moja, mkoani Pwani, watoto hao walisema ndani ya jengo hilo kuna watoto wengi wa kike na kiume.

Walisem a   w atoto hao wanafanyishwa kazi na kuteswa kwa kutandikwa fimbo, kuchomwa moto na kupigwa shoti ya umeme hasa wanapowaulizia wazazi wao ambapo baadhi yao hubakwa na kulawitiwa.

"Jumba hili limejengwa ndani ya handaki, tulikuwa tukifanyishwa kazi ngumu na nzito, usiku tunajaza maji katika mapipa mengi na kubebeshwa ndoo kupanda na kushuka kilima.

"Tunapigwa fimbo, wasichana wanafungiwa kwenye vyumba, wanabakwa na kulawitiwa kwa zamu na Wazungu, tunachomwa moto (alionesha mguu wake uliochomwa) na kupigwa shoti ya umeme tunapowaulizia wazazi wetu," alisema Emmanuel kwa uchungu akitokwa na machozi.

Aliongeza kuwa, asubuhi ya Novemba 23 mwaka huu, katika jengo hilo kulitokea kutokuelewana kati ya Wazungu na Waswahili ambapo mswahili mmoja aliwatisha wazungu kwa kuwaambia polisi wanakuja hivyo walikimbia na kuacha mlango wazi.

"Hali hiyo iliniwezesha mimi, mdogo wangu na watoto wengine wachache waliokuwa na nguvu kufanikiwa kutoroka, nilimshika mkono mdogo wangu ambaye alionekana kuchoka nikamvuta.

"Watoto wengine wachache waliokuwa na nguvu nao wakatoka, wengi hawakuweza kutoka kutokana na kukosa nguvu, wanaumwa, wana vidonda vikubwa mwilini kutokana na kuchomwa moto na kupigwa shoti ya umeme, wasichana hawakuweza kabisa kutoka kwa kuwa wamefungiwa ndani ya vyumba," alisema Emmanuel

Aliongeza kuwa , alijikokota taratibu na mdogo wake mbali ya maumivu makali waliyonayo akatokea Mswahili mmoja ambaye alikuwa na gari lenye vioo vyeusi akawaambia wapande ili awatoroshe.

"Tulipanda gari hilo akatushusha darajani mpakani mwa Manispaa ya Kinondoni na Wilaya ya Kibaha, jirani na mzani eneo ambalo sisi hatukuwa tukilifahamu...dereva huyo alituambia gari limeishiwa mafuta hivyo alitutaka tumsubiri aende kuyanunua.

"Tulitembea kidogo tukiwa hatujui tunakokwenda... tulikaa kando ya barabara kutokana na uchovu pamoja na njaa kali kwani katika jengo hilo mbali na kazi nzito tulizokuwa tukizifanya na mateso mengi, mlo ulikuwa mmoja tu kwa siku.

"Tulikula saa 10 jioni, wali na maharage...tukiwa kando ya barabara, nilisikia sauti ya baba yangu wa kufikia, dereva wa magari makubwa yanayobeba kokoto ikiniita.

"Nilidhani naota kumbe ilikuwa kweli, alikuja akatukumbatia akalia kwa uchungu kwa namna tulivyokuwa tumechoka na afya kuzorota, akatupeleka polisi ambapo tulipatiwa maji tukaoga na kupewa chakula kizuri na kitamu, tukala na kupata nguvu za kuzungumza vizuri," alisema Emmanuel.

Akizungumza na Majira, Emmanuel alisema baada ya kutekwa yeye na mdogo wake, walifungwa na vitambaa vyeusi usoni hadi walipofikishwa ndani ya jumba hilo la mateso.

Aliiomba Serikali kufanya jitihada za hali na mali ili kuwaokoa watoto wengine waliopo katika jengo hilo.

Mama mzazi wa watoto hao, Martha Godianus (29), ambaye anafanya shughuli za mama lishe, njia panda y a Ba r a k u d a , Ta b a t a Manispaa ya Ilala, alisema amehangaika zaidi ya miezi mitatu kuwatafuta watoto hao bila mafanikio.

"Nimepoteza fedha nyingi kwa kuwatafuta na kutapeliwa mara kadhaa katika kuhangaika," alisema Godianus huku akitokwa na machozi ya furaha katika Kituo kidogo cha Polisi Maili Moja.

Alisema zaidi ya watoto saba walipotea katika mtaa wao, wawili wakapatikana baada ya wiki mbili, wengine wakiwemo wanaye wakawa hawajapatikana na kuomba Serikali ilichukulie kwa uzito suala hilo ili kubaini kundi linalowateka watoto na kuwatesa.

Kamanda wa Polisi mkoani Pwani, Ulrich Matei alikiri kutokea kwa tukio hilo na kuanza kulifanyia kazi kwa kushirikiana na Jeshi la Polisi Mkoa wa Kipolisi Kinondoni, Dar es Salaam.

Alisema makachero wa polisi wamewahoji watoto hao ili kupata maelekezo ya kufika katika andaki hilo na kuwataka watu wote wenye taarifa za eneo hilo watoe ushirikiano.


-Gazeti la Majira

Saturday, November 23, 2013

Binti auawa Kimara, Dar kwa mpenzi wake akisubiri matokeo ya kidato cha nne

Mwanafunzi aliyehitimu kidato cha nne mwaka huu, Sharifa Abdallah (18) ameuawa kwa kuchomwa kisu shingoni na mbavuni chumbani kwa mvulana aliyedai  kuwa mpenzi wake maeneo ya Kimara Golani, Dar es Salaam.

Tukio hilo lilitokea juzi saa 8:30 mchana na baadaye mvulana huyo aliyetambuliwa na Polisi kwa jina la Abdul Alpha (22) kujisalimisha katika kituo cha Polisi cha Stendi Kuu ya Mabasi yaendayo mikoani cha Ubungo, akidai alikuwa akitaka kutoroka lakini aliona amefanya dhambi kubwa.
Akizungumza na mwandishi jana, mama mkubwa wa marehemu, Mwajuma Khamis alisema Sharifa alimaliza kidato cha nne katika sekondari ya Luguruni na alikuwa akisubiri matokeo.
Alisema juzi waliporejea kutoka kazini hawakumkuta nyumbani, waliulizia kwa ndugu kutokana na kwamba hakuwa na tabia ya kutoka nyumbani, lakini hawakufanikiwa kumpata hadi jioni ndipo polisi walipowataarifu kupatikana kwa mwili wake.
Alisema mwili wa marehemu ulikutwa chumbani kwa kijana huyo karibu na nyumbani kwao ukiwa na majeraha mwilini, lakini hawakujua kama mtoto wao ana mwanaume, wanatarajia kumzika kesho saa saba mchana.
Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Kinondoni, Camilius Wambura alisema polisi walipata taarifa za tukio hilo katika kituo cha Ubungo na kwenda katika chumba cha kijana huyo kilichokuwa kimefungwa kwa ndani na kukuta mwili wa msichana huyo ukiwa umejeruhiwa.
Alisema baada ya kumhoji mtuhumiwa, alisema alifanya hivyo kutokana na wivu wa kimapenzi, kwani alikuwa na uhusiano na msichana huyo lakini wazazi wa msichana hawakutaka amwoe, hivyo kumtaarifu kuwa amepata mchumba mwingine.
Alipoulizwa kwa nini hakutoa taarifa katika kituo cha Polisi Kimara alikofanyia mauaji, alisema aliogopa watu wa maeneo yale wangempiga na kumwua, kwa kitendo hicho.
Mwili wa marehemu umehifadhiwa katika hospitali ya Tumbi, Kibaha, huku kijana huyo akishikiliwa na Polisi.

Wednesday, November 20, 2013

Mchungaji wa kanisa la Pentekoste awabaka wanafunzi wawili na kuwaambukiza KASWENDE huko jijini Mbeya..!!


Wanafunzi  waliobakwa  kwa  zamuBaadhi ya walimu wa shule ya Msingi Maendeleo wakizungumza kwa hisia tukio hilo la ubakaji lililofanywa na MchungajiKanisa linaloendeshwa na Mchungaji Bryson MwaikamboShule ya Msingi Maendeleo ambako wanasoma wasichana wanaodaiwa kubakwa na Mchungaji kwa zamuWazazi wa watoto wanaodaiwa kubakwaNyumba anayoishi Mchungaji Mwaikambo ikiwa imepigwa kufuri huku mwenyewe akiwa ''amelala mbele!! baada ya kufanya unyama wake

****************************************

MCHUNGAJI wa kanisa la Pentekostal aliyefahamika kwa jina la Bryson Mwaikambo(55) anadaiwa kuwabaka na kuwaambukiza ugonjwa wa zinaa wanafunzi wawili wa kike wanaosoma katika shule ya msingi ya Maendeleo wa  kata ya Nsalala wilaya ya Mbeya vijiji mkoani Mbeya.
 
Wanafunzi hao (majina yanahifadhiwa) wenye umri kati ya miaka 11 na 13 wanaosoma darasa la nne na darasa la sita walifanyiwa unyama huo kuanzia mwaka 2012 ambapo alianza kujenga mazoea na watoto hao wadogo kwa kuwapa peremende  pamoja  na fedha.
 
Imeelezwa kuwa mchungaji huyo ambaye anaendesha ibada katika kanisa hilo dogo lenye waumini wachache lililopo kitongoji cha kanani kijiji cha ‘Tunduma Road’ alikuwa akiwavizia watoto hao kwa muda mrefu kila walipokuwa wanapita kuelekea shuleni.
 
Katika jitihada zake za kuwanasa watoto hao wa kike alimdanganya mmoja wa wazazi wa watoto aliyefahamika kwa jina la Bw.John Mussa(38) na kumuomba binti yake awe anamsaidia kazi za nyumbani nyakati za jioni kutokana na kuwa  mke wa mchungaji kuwepo safarini.
 
Kwa kuamini kuwa mchungaji huyo alikuwa ni mtumishi wa Mungu, Bw. Mussa aliridhia mwanaye aende kuishi na Mtumishi huyo wa Mungu bila kujua hatima ya kile ambacho kimemtokea binti yake kwa sasa.
 
Kwa mujibu wa maelezo kutoka kwa wazazi na walimu wa shule ya Msingi Maendeleo ni kwamba mabinti hao walikuwa wakifanya ngono na mchungaji huyo kwa zamu na kwamba walianza kujua tatizo hilo baada ya kutokea mgongano baina ya wasichana hao wawili .
 
‘’Tumejua tukio hili baada ya kutokea ugomvi baina yao wa kugombania maji na hivyo kuanza kurushiana maneno, mmoja wa watoto hao alikuja ofisini kushitaki kuhusu ugomvi wao ndipo mmoja akasema kuwa mwenzie anatembea na Mchungaji Mwaikambo’’alisema Mwalimu mkuu msaidizi Bi. Lucy Kamongile.
 
Alifafanua kuwa, baada ya tukio hilo walimu kwa pamoja walilazimika kuwauliza zaidi ndipo walipoanza kujieleza kuwa wamekuwa wakilala na Mchungaji huyo kwa muda mrefu na kwamba mwanzo alikuwa akiwapa peremende na baadaye akaanza kuwapa fedha.
 
Alisema kuwa walilazimika kuitisha kikao cha dharura baina ya wazazi wa watoto hao na walimu ambapo walieleza tukio zima la kuingiliwa kimwili na Mchungaji huyo tangu mwaka jana.
 
‘’Nililazimika kuwaita wazazi pamoja na wanafunzi tulikaa katika ofisi ya walimu, watoto walieleza tukio zima mbele ya wazazi wao juu ya vitendo walivyokuwa wakifanyiwa na Mchungaji huyo."Alisema  mwalimu  mkuu  msaidizi
 
Alisema kuwa mara baada ya kikao hicho cha wazazi waliwapeleka watoto hao katika kituo kidogo cha Polisi kilichopo  katika mji  mdogo wa Mbalizi ambako walipewa Fomu ya Polisi Na. 3,(PF3) kwa ajili ya kuepelekwa hospitali ili wapatiwe matibabu.
 
Mwalimu Kamongile ambaye alikuwa na walimu wenzie katika ofisi ya Mwalimu mkuu wa shule hiyo wakati akitoa taarifa hizi mbele ya Ripota Wetu kuwa wanafunzi hao walipatiwa matibabu katika hospitali Teule ya Ifisi ambapo kwa mujibu wa taarifa za mganga aliyewachunguza  watoto hao ni kwamba mbali na kufanyiwa ubakajiwote wawili walikuwa wameambukizwa ugonjwa wa zinaa wa kaswende.
 
‘’Tukio hili limetufedhehesha sana tulikuwa tunatafakari wapi tutaenda,tunaomba kilio chetu kifike chama cha Waandishi wa Habari wanawake TAMWA kitoe taarifa hizi kwa undani waone namna ambavyo jamii ya pembezoni inavyokosa msaada na haki za kisheria,’’alisema Mwalimu Kamongile.  
 
Mwalimu huyo alisema kuwa wanatambua juhudi za chama cha waandishi wa habari wanawake TAMWA ambazo wamekuwa wakizifanya hivyo wanaimani chama hicho kikisikia suala kitalifanyia kazi kwa kina zaidi kuisaidia jamii ambayo aina mahali pa kusemea.
 
Kwa upande wa watoto hao ambao walikuwa wakizungumza kwa kupokezana juu ya kadhia iliyowakuta walisema kuwa Mchungaji huyo alianza kufanya nao vitendo vya ngono tangu mwaka 2012 kwa kuwadanganya kwa fedha na peremende na baadaye wakazoea kwenda kwa Mchungaji huyo mara kwa mara.
 
Mwanafunzi anayesoma darasa la nne alisema kuwa alianza kutembea na Mchungaji huyo wakati akimpitia mwenzie aliyekuwa akiishi nyumbani kwa mchungaji ambapo siku hiyo alimuita chumbani kwake na kumlazimisha kulala kitandani ambapo alianza kumuingiza vidole katika sehemu zake za siri.
 
“Siku ya kwanza nililia sana wakati mwenzangu yupo pembeni akishuhudia mchungaji akinifanya na ndipo mwenzangu alisema jikaze rafiki yangu”alisema Mtoto huyo.
 
Alisema kuwa mara baada ya kumuingiza vidole alivua nguo zake na kumbaka huku akilia wakati msichana mwenzie (alimtaja jina) akiwa amekaa pembeni ya kitanda akimweleza kuwa aache kulia kwa kuwa baada ya kumaliza watapewa fedha za kutumia shuleni.
 
Binti huyo aliendelea kusema kuwa alipata maumivu makali wakati Mchungaji huyo akitekeleza ubakaji wake ambapo mara baada ya kumaliza` alimpa sh.500 na peremende na baadaye alimwita mwenzie kitandani na kufanya naye ngono huku akishuhudia kwa macho yake.
 
Alisema mara baada ya kumaliza kufanya na mwenzie Mchungaji Mwaikambo aliwaonya wasiseme kwa wazazi wao kisha akawapa fedha na kuwaonya wasiseme jambo hilo kwa mtu yoyote.
 
Akizungumza sababu za kutosema kwa walimu au wazazi wake binti mwingine anayesoma darasa la sita alisema kuwa Mchungaji huyo aliwatishia kuwachinja na kuwafukia kwenye shimo iwapo atasikia wamesema tukio hilo kwa wazazi ama walimu wao.
 
Alisema kuwa Mchungaji aliwaomba wazazi wake ili aende kuishi nyumbani kwake kumsaidia kazi kutokana na mama Mchungaji ‘’Mke wa Mchungaji’’ kuwa safarini na kwamba katika siku hizo ndipo Mchungaji huyo alipoanza kulala naye mahusiano taratibu.
 
Alisema kwa siku za mwanzo alikuwa akimuingiza vidole katika sehemu zake za siri na baadaye akaanza kumbaka ambapo alijisikia maumivu makali lakini alimbembeleza kwa kumpa sh.1000 ambayo alikuwa akitumia shuleni kwa kununua chipsi.
 
‘’Alikuwa akiniingiza vidole huku chini(akionyesha sehemu za siri) akanibaka, sikuweza kumwambia baba niliogopa atanichinja..mwenzangu alipokuwa anakuja kunipitia kwenda shuleni naye alianza kumuingiza vidole akambaka!!, alilia sana, nikamwambia asilie atatupa hela,’’alisema.
 
Alisema kuwa wamebakwa na Mchungaji huyo zaidi ya mara nne na kila alipokuwa akiwabaka alikuwa anawapa hela za kutumia shuleni.
 
Kwa upande wazazi wa watoto hao Bw.Suveli Harrison na Bw. John Mussa walikiri kuitwa shuleni na kupata taarifa za kubakwa kwa watoto wao walipoitwa shuleni ambapo watoto walijieleza walichokuwa wakifanyiwa na Mchungaji Mwaikambo mbele ya walimu.
 
‘’Jambo hili lilitushitua sana, machozi yalitulenga, hatukutegemea kusikia Mchungaji anaweza kuwabaka watoto ambao ni sawa na wajukuu zake, tulienda polisi walitupa karatasi tukaenda Hospitali ya Ifisi, watoto walikutwa na maambukizi ya ugonjwa wa zinaa,’’alisema Bw. John Mussa.
 
Alisema kuwa yeye aliridhia mwanaye kuishi na Mchungaji huyo baada ya kuombwa kutokana na mchungaji huyo kuishi na mtoto mdogo wakati mkewe akiwa safarini.
 
Bw. Mussa alisema kuwa hakujua kuwa kama kuna siku mwanaye atadhurika kwa kufanyiwa kitendo cha unyanyasaji na ukatili wa kijinsia kama walivyofanyiwa watoto hao na kwamba hata hivyo hadi sasa hakuna jitihada zozote za jeshi la polisi zilizofanikisha kumnasa Mchungaji huyo.
 
Alisema kuwa kwa sasa watoto hao wamekuwa wakitishiwa na Mchungaji kutokana na kufahamika kuwa yeye aliwabaka na kwamba anaomba msaada wa kisheria kusimamia haki ili sheria iifuatwe dhidi ya mtuhumiwa wa ubakaji.
 
Naye mzazi mwingine Bw.Suvile Harrison alisema kuwa hakujua chochote juu ya vitendo alivyofanyiwa mwanaye na Mchungaji huyo na  kwamba alifahamu tukio hilo baada ya kuitwa shuleni ambako walimu waliwaita watoto wao na kueleza tukio zima walilokuwa wakifanyiwa na Mchungaji.
 
Alisema kuwa hakubaini mabadiliko yoyote kwa mwanaye juu ya vitendo alivyofanyiwa na wala hajawahi kuhisi lolote hadi hapo alipoitwa shuleni na walimu.
 
Baada ya taarifa hizo waandishi wetu wa habari  walifunga safari hadi katika nyumba ambayo inasadikiwa kuwa ndipo anapoishi Mchungaji huyo na kukuta mlango ukiwa umefungwa lakini alijitokeza jamaa ambaye alijitambulisha kuwa ni mmiliki wa nyumba hiyo Bw. Zacharia Gambi.
 
Bw.Gambi alisema kuwa anamfahamu mpangaji wake kwa jina moja la Mchungaji Mwaikambo na kwamba mbali ya kuwa ni Mchungaji wa Kanisa la Kipentekoste ni Balozi wa nyumba kumi wa mtaa wa Kanani.
 
Bw.Gambi alisema kuwa Mchungaji huyo hajaonekana muda mrefu na kwamba mkewe amekuwa na desturi ya kuondoka alfajiri kuelekea shambani na kurudi usiku.
 
Kadhalika imeelezwa na baadhi ya watu ambao hawakupenda kutajwa majina yao  kuwa  kitendo cha Mchungaji huyo kuwabaka mabinti wadogo kimetokana na imani za nguvu za giza kwamba kwa kufanya hivyo kitamuongezea waumini katika kanisa lake dogo lililopo katika mtaa wa Kanani.
 
Mama mzazi wa mmoja wa watoto waliobakwa aliyejitambulisha kwa jina la Jane John(35) alisema kuwa awali yeye alikuwa ni mmoja wa waumini katika kanisa hilo lakini baadaye walihamia kanisa jingine baada ya kuona mienendo ya mchungaji huyo kutofanana na kazi ya huduma za kiroho.
 
Alisema waumini wengi wamehama katika kanisa hilo wakiwemo watoto wake wakubwa wa kike ambao walieleza waziwazi tabia ya ukware ya Mchungaji huyo ya kuwafuatilia mabinti wadogo kwa ajili ya kufanya nao vitendo vya ngono.
 
Diwani wa Kata ya Nsalala iliyopo Mbeya vijijini Bw.Mashauri Mbembela alipozungumza na waandishi wa gazeti hili alisema kuwa anashangazwa tukio hilo kutoshughulikiwa kwa kipindi chote huku taarifa zikiwa zimefikishwa kituo cha polisi.
 
Alisema kuwa tukio hilo ni la unyanyasaji ambalo lilipaswa kushughulikiwa kwa nguvu zote na kwamba kuna haja ya kuweka sheria ngumu itakayokomesha vitendo vya ubakaji kwa watoto wa kike.
 
Bw.Mbembela alisema kuwa ili kukomesha tabia za ubakaji, itungwe sheria ya kuwahasi wabakaji badala ya kuwafunga jela miaka 30  ambako wanaenda kula chakula kinachotokana na kodi za wananchi.
 
‘’Wabakaji wanafungwa jela, wakimaliza vifungo vyao hurejea uraiani ambako wanaweza kuendeleza vitendo hivyo, njia pekee ya kukomesha ubakaji ni kuwahasi, wakirudi uraiani wataendeleza kujenga Taifa,’’alisema Bw. Mbembela.
 
Ripota wetu alifanya jitihada za kutafuta namba za simu za mchungaji huyo ambaye mara baada ya kupokea na kuulizwa juu ya tuhuma hizo alikanusha na kusema kuwa huu ni uzushi na uongo uliolenga kumpaka matope ili kuchafua huduma zake anazotoa kwa waumini .
 
Alidai kuwa kanisa lake la Pentecostal Holiness lenye  jumla waumini nane linatoa huduma za uhakika kijijini hapo hivyo baadhi ya wafuasi wa shetani wanalipiga vita ili lisiendelee kukua ili kuwafikia wanakondoo wengi.
 
“Wananipakazia tu unaweza kuingiwa na ibilisi na hivi ulivyonipigia nafikiria kuchukua maamuzi magumu na mwili wangu hamtauona kamwe bora uliwe na ndege  na wanyama wa porini  niende jehanamu kuliko kuchafuliwa huku”alisema Mchungaji huyo.
 
Alisema kuwa tuhuma hizo zimeelekezwa kwake baada ya kumdai fedha mmoja wa wazazi wa watoto hao ambaye alikuwa akifanya kibarua cha kujenga ofisi ya kata ambapo mama huyo alimkopesha fedha sh.5000 na alipoanza kudai ndipo akaanza kuzushiwa tuhuma hizo.
 
Hata hivyo alisema  Jumanne iliyopita alifuatwa na askari mgambo sita wenye virungu ambao walitaka kumkamata lakini kwa nguvu za yesu walishindwa na kuondoka zao.
 
“Mimi naishi kwa nguvu za Yesu mtu yeyote mwenye nia mbaya na mimi hawezi kunipata nataka niwe kama mfalme aliyejitoa mhanga nijiue mwili wangu usionekane duniani”alisisitiza na kukata simu. 
 

Kamanda wa polisi mkoa wa Mbeya Bw.Diwani Athumani alisema kuwa amepata taarifa hizo za ubakaji ambapo amemuagiza Ofisa Upelelezi wa Mkoa Bw.Mtatiro Nyamuhanga ambaye atalifuatilia kwa karibu tukio hilo na kwamba hata hivyo mtuhumiwa bado hajatiwa mbaroni.