Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akisalimiana na wakuu wa
vyombo vya ulinzi na Usalama wa Uganda muda mfupi baada ya kuwasili
katika uwanja wa ndege wa Entebbe nchini Uganda kuhudhuria mkutano wa
wakuu wa nchi za jumuiya ya Afrika Mashariki.
*****************
Wakuu
wa nchi zinazounda jumuiya ya Africa Mashariki wanakutana leo tarehe 30 Novemba huko
Kampala, Uganda.
Wakuu hao ni pamoja na Rais Jakaya Kikwete wa
Tanzania, Yoweri Mseveni wa Uganda, Paul Kagame wa Rwanda, Pierre
Nkuruzinza wa Burundi na Uhuru Kenyatta wa Kenya.
Masuala
watakayozungumzia leo ni pamoja na soko la pamoja, umoja wa forodha,
shirikisho la kisiasa na umoja wa sarafu ambapo leo watatia saini
mkataba wa kuwa na sarafu moja