Saturday, November 30, 2013

Rais Kikwete awasili jijini Kampala kuhudhuria mkutano wa EAC....Maada kuu watakazoongelea ni pamoja na Sarafu moja ya jumuiya ya Afrika Mashariki

Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akisalimiana na wakuu wa vyombo vya ulinzi na Usalama wa Uganda muda mfupi baada ya kuwasili katika uwanja wa ndege wa Entebbe nchini Uganda kuhudhuria mkutano wa wakuu wa nchi za jumuiya ya Afrika Mashariki.
*****************

Wakuu wa nchi zinazounda jumuiya ya Africa Mashariki wanakutana leo tarehe 30 Novemba huko Kampala, Uganda.

 Wakuu hao ni pamoja na Rais Jakaya Kikwete wa Tanzania, Yoweri Mseveni wa Uganda, Paul Kagame wa Rwanda, Pierre Nkuruzinza wa Burundi na Uhuru Kenyatta wa Kenya.
 
 Masuala watakayozungumzia leo ni pamoja na soko la pamoja, umoja wa forodha, shirikisho la kisiasa na umoja wa sarafu ambapo leo watatia saini mkataba wa kuwa na sarafu moja