Tuesday, November 5, 2013

HII NDIO MBINU MPYA WANAYOITUMIA "WAUZA UNGA "KUSAFIRISHA MADWA YA KULEVYA.....

 


Wakati Naibu Spika, Job Ndugai akisema maelezo binafsi ya Mbunge wa Viti Maalumu, Esther Bulaya (CCM) kuhusu biashara ya dawa za kulevya na athari zake aliyoyatoa bungeni juzi jioni hayatajadiliwa, Kitengo cha Kudhibiti Dawa za Kulevya nchini kimeshtukia mbinu mpya zinazotumiwa na wafanyabiashara wa dawa za hizo.
Ndugai alitoa ufafanuzi huo jana baada ya Mbunge wa Mwibara (CCM), Kangi Lugola kuomba mwongozo jana, akitaka Bunge likubali mjadala wa suala hilo kutokana na unyeti wake.
Akizungumza na Mwananchi Dar es Salaam jana, Kamanda wa kitengo hicho, Godfrey Nzowa alisema wameshtukia mbinu mpya zinazotumiwa na wafanyabiashara wa dawa za kulevya, ambao sasa wanatumia barabara badala ya anga.
“Mfano mzuri, tumeshtukia usafirishaji wa epedrine na Juni 24 mwaka huu, Saada Ally Kilongo (26) alikamatwa Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere na kilo 11,000 za dawa za kulevya aina ya epedrine, ambazo ni mali ghafi za thamani zaidi ya Sh170 mil,” alisema.

SOURCE:MWANANCHI