Monday, July 8, 2013

UGONJWA WA KIPINDUPINDU WALITIKISA JIJI LA MBEYA...MIKUSANYIKO YAPIGWA MARUFUKU


UGONJWA wa kipindupindu, umeingia katika wilaya ya Kyela na kuua watu wawili na 39 wakiwa wamelazwa.

Taarifa zinasema ugonjwa huo umeibuka wilayani humo wiki iliyopita ukisadikika kuanzia katika Kijiji cha Ngonga na kisha kusambaa hadi Kilwa.

Kutokana na hofu ya kupata maambukizi kwa wananchi wengine, serikali imepiga marufuku mikusanyiko ikiwemo ya harusi, kipaimara, ngoma, michezo na sikukuu inayosherehekewa kila mwaka ya wakulima.