Friday, July 26, 2013

POLISI YAKAMATA MILIPUKO NA SILAHA JIJINI DAR

   Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Kinondoni, ACP Camillius Wambura akionesha baadhi ya milipuko iliyokamatwa.
…Kamanda Wambura akionyesha silaha mbili za moto zilizokamatwa kwa mama huyo.
   … Vitu hivyo vya hatari vikionekana kwa ukaribu.
   …Viroba vyote hivi vimejaa milipuko.
    …Kamanda Wambura akifafanua jambo kwa waandishi wetu (hawapo pichani).
POLISI katika Mkoa wa Kipolisi wa Kinondoni wamemkamata mwanamke mmoja aitwaye Rozi Amel (45) ambaye ni mfanyabiashara akiwa na milipuko, baruti na viunganishi vyake pamoja na silaha mbili za moto huko Salasala IPTL jijini Dar. Haikuweza kufahamika mara moja milipuko hiyo alikuwa akiipeleka wapi. Kwa mujibu wa  Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Kipolisi Kinondoni, ACP Camillius Wambura upelelezi bado unaendelea.