Friday, July 26, 2013

MTU MMOJA AFARIKI KWA KUPIGWA RISASI DAR


Wananchi wakibeba mwili wa marehemu baada ya kuuawa kwa kupigwa risasi na watu wasiojulikana.
Mwanaume mmoja ambaye hakujulikana jina lake mara moja, muda mfupi uliopita ameuawa kwa kupigwa risasi na watu wasiojulikana eneo la Tegeta jijini Dar es Salaam. Kwa mujibu wa mashuhuda wa tukio hilo, 
wauaji ni wanaume wawili waliokuwa katika pikipiki maarufu kama 'Bodaboda'. Marehemu alikuwa akishuka katika gari lake aina ya Toyota Mark II yenye namba za usajili T 508 ADY ndipo alipopigwa risasi kadhaa.