KWELI mapenzi yanaua! Mwanaume mmoja aliyetajwa kwa jina la Dotto, anahusishwa na mauaji ya mkewe, Zainab Bakari, mkazi wa Vingunguti jijini Dar es Salaam.
Tukio hilo la kusikitisha lilijiri hivi karibuni maeneo hayo ambapo Dotto alidaiwa kumchoma mkewe huyo kisu na kusababisha kifo chake baada ya mama watoto wake huyo kukataa kurudiana naye ili ampikie futari katika kipindi hiki cha Mfungo wa Mwezi Mtukufu wa Ramadhani.
Akizungumza na wanahabari wetu, dada wa marehemu aliyejitambulisha kwa jina la Asia Hatibu alisema kabla ya tukio hilo, marehemu Zainab na mumewe Dotto walikuwa mke na mume wa ndoa lakini baadaye walitengana kiaina (bila talaka).
Alisema siku ya tukio hilo, Dotto alimfuata Zainab nyumbani kwa wifi yake alikokuwa akiishi na kumuomba warudiane lakini mwanamke huyo alikataa.
Akizungumza na wanahabari wetu, dada wa marehemu aliyejitambulisha kwa jina la Asia Hatibu alisema kabla ya tukio hilo, marehemu Zainab na mumewe Dotto walikuwa mke na mume wa ndoa lakini baadaye walitengana kiaina (bila talaka).
Alisema siku ya tukio hilo, Dotto alimfuata Zainab nyumbani kwa wifi yake alikokuwa akiishi na kumuomba warudiane lakini mwanamke huyo alikataa.