Monday, December 9, 2013

Video: Kijana Ajiua Huko Nchini Kenya mara baada ya Manchester kufungwa Goli 1-0 na Newcastle Utd Ukiwa ni Mwendelezo wa matokeo mabaya ya timu Hiy


Meneja mpya wa Manchester United, David Moyes anaendelea kukabiliwa na kibarua kizito kutokana na kikosi chake kuendelea kufanya vibaya tangu akabidhiwe mikoba na meneja wa zamani, Alex Ferguson. Hii ni baada ya kijana mmoja anayeaminika kuwa shabiki wa timu hiyo kujiua juzi. Dec 7 jijini Nairobi, Kenya baada ya timu yake kufungwa 1-0 na Newcastle.





Polisi wamesema kijana huyo aitwaye, John Jimmy Macharia, 23, alijirusha kutoka ghorofa ya 7 baada ya kujua timu yake imepoteza mchezo huo.
“Mashahidi wote waliokuwepo wakati wa tukio bado wapo mikononi mwa polisi wanahojiwa,” alisema.
Naye rafiki wa karibu wa marehemu alisema kabla ya kuanza kwa mpira marehemu John ,aliwaambia rafiki zake yeye hawezi kuangalia game kwenye banda la video anaenda kuangalia nyumbani kwake.
Source:KTN