Baada ya kusimamisha shughuli za maandalizi ya muendelezo wa saba ya
Filamu ya Fast and Furious kutokana na kifo cha muigizaji 'Paul Walker
aliyefariki mwishoni mwa mwezi uliopita kwa ajali ya gari.
Leo Desemba 23 Muigizaji na mkuu wa filamu ya Fast na Furious,Vin
Diesel ametangaza rasmi tarehe ya kutoka kwa muendelezo wa saba wa
filamu hiyo yenye mafanikio
makubwa.
Kupitia ukurasa wake wa Facebook, Diesel ameweka picha akiwa na Paul Walker na
kuandika kuwa hiyo ilikuwa scene yao ya mwisho kuwa na staa huyo na
kutangaza rasmi kuwa Fast and Furious sehemu ya 7 itatoka April 10 mwaka 2015.
“The last scene we filmed together…
There was a unique sense of completion, of pride we shared… in the
film we were now completing… the magic captured… and, in just how far
we've come… Fast and Furious 7 will be released… April 10th 2015! P.s.
He'd want you to know first…,” ameandika Diesel.