Mswada huo awali ulishtumiwa na makundi ya kutetea haki pamoja na serikali za Magharibi ikiwemo Marekani kwa sababu ulijumuisha adhabu ya kifo.

Mswada uliopitishwa Ijumaa unatoa adhabu ya kifungo cha maisha jela kwa yeyote atakayehukumiwa kwa kile ilichosema ni "vitendo vilivyopita mipaka" vya ngono kati ya watu wa jinsia moja.
Waziri Mkuu Amama Mbabazi alikaririwa akisema kuwa serikali ya Uganda itafanya mashauriano zaidi kuhusu mswada huo ambao unahitaji kutiwa saini na Rais Yoweri Museveni kabla ya kuwa sheria kamili nchini humo.
Sikiliza Audio hapo