Monday, November 4, 2013

VIDEO:WATU 6 MBARONI KWA KUMCHARANGA MAPANGA DKT MVUNGI


Video ikimwonyesha Kamanda Kova wakati akiongea na wanahabari kuhusu matukio mbalimbali ya kihalifu na watuhumiwa waliokamatwa na Jeshi la Polisi wakiwemo waliomshambulia Dk. Mvungi.
Kamanda Suleiman Kova akiongea na wanahabari kuhusu wahalifu mbalimbali waliotiwa nguvuni na Jeshi la Polisi.
Baadhi ya vitu walivyokutwa navyo wahalifu katika matukio mbalimbali jijini Dar es Salaam.
Stori: Jelard Lucas na Chande Abdallah
WATU 6 wanashikiliwa na jeshi la polisi kwa kuhusika na tukio la kumshambulia Dkt. Sengondo Mvungi aliyevamiwa na majambazi nyumbani kwake Kibamba Msakuzi juzi.
Akizungumza na waandishi wa habari Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Selemani Kova amesema katika operesheni maalum iliyofanywa na jeshi la polisi, wamefanikiwa kuwakamata watu sita ambao majina yako yamehifadhiwa kwa sababu za usalama. Aidha Kamanda Kova aliongeeza kuwa bado hawajapata uthibitisho kamili juu ya sakata hilo na uchunguzi unaendelea kuwabaini wahusika halisi wa shambulio hilo