Saturday, November 30, 2013

SAKATA LA KUPIGA PICHA ZA UCHI ASHA KULIPWA MIL.500 ......

Kampuni ya Global Publishers Ltd, inayochapisha magazeti ya Uwazi, Championi, Ijumaa Wikienda, Risasi, Amani na gazeti hili, iko tayari kumlipa kiasi cha shilingi Milioni mia tano, mnenguaji wa Bendi ya Twanga Pepeta, Aisha Mohamed Mbegu ‘Aisha Madinda’ ikiwa atatoa uthibitisho kwamba, picha za utupu alizopigwa nchini Afrika Kusini ni za kutengenezwa, soma data chini.

Ofa hii imekuja siku mbili baada ya gazeti moja la michezo na burudani linalotoka mara mbili kwa wiki, toleo la Jumanne Mei 18, 2010 kuchapisha makala kuhusu Aisha akikanusha kuwa, picha zile si zake na kwamba zilitengezwa na mbaya wake kwa lengo la kumchafua jina.
...kulia kwake ni unga..bila shaka ulimpotezea kumbukumbu

Hata hivyo, katika makala hayo, Aisha alishindwa kuthibitisha picha hizo ni za kutengeza, zilitengnezwa wapi na lini na vigezo gani vinavyoonesha picha hizo ni za kutengeneza.

Ushahidi wa Global kuwa, picha hizo ambazo za mnato na video ni za Aisha mwenyewe upo wazi na hakuna shaka yoyote.

Moja ya ushahidi huo, katika picha za video, kuna sehemu Aisha anaongea kwa tambo akiwaponda watu wanaomfuatafuata na kumsema vibaya.
...sasa hapa inakuwaje picha hizi zikitoka gazetini...!!!!
Tunamnukuu: “Wanasema eti nimeishiwa, nimekosa nauli ya kurudi Tanzania, waende basi kwa huyo Asha Baraka wakaseme, maana wamezidi kwa maneno.” 

Hata hivyo, sehemu kubwa ya picha za mnato na video hizo zinaonesha wazi kwamba, Aisha alikuwa tayari kupigwa picha hizo, kwani kuna wakati alikuwa akitazama kamera na nyingine akiwa ameweka pozi.
......aaa jamani...niacheni ki mpango wangu!!!!

Aidha, ushaidi mwingine kuwa picha hizo ni Aisha, mara baada ya kutua Bongo akitokea Afrika Kusini, alimwangukia bosi wake, Asha Baraka akimwomba radhi kwa yote aliyoyafanya Afrika Kusini ambapo gazeti hili liliripoti likiwa na kichwa cha habari; NATESEKA.

Katika habari hiyo, Asha Baraka ‘Iron Lady’ alinukuliwa akisema kuwa, anaamini Aisha aliteleza na hivyo ameamua kumsamehe na kumrudisha kundini kuendelea kupiga mzigo kama kawa.
....ntajua ntakachowaeleza watanzania....

Tunamnukuu Asha Baraka: “Mimi kwa Aisha ni kama mama au dada yake, na ninavyojua, mtoto anapojisaidia kiganjani mzazi huwezi kuukata mkono bali utausafisha kisha kuyaacha mambo yaendelee. Vivyo hivyo kwa Aisha, kafanya kosa lakini hakuna kosa lisilostahili msamaha, kwahiyo asamehewe.

“Atakachokifanya Aisha ni kuomba radhi kwa mashabiki wake na katika kila sehemu ambayo tutafanya shoo atafanya hivyo kabla ya kuanza kutumbuiza.” 
.......ni mzimu wangu tu huu...siyo mimi..!

Pia, katika kuonesha ubinadamu, mwisho wa habari hiyo Mhariri aliwaomba Watanzania wasahau yaliyopita kuhusu Aisha na aombewe kwa Mungu ili amwepushe na mitihani mingine nkatika maisha yake.

Katika hali ya kushangaza sana, baada ya kimya cha muda mrefu, Aisha ameibuka katika gazeti hilo akidai kwamba picha zile zilikuwa za kutengeneza hali iliyozua maswali miongoni mwa wasomaji wetu.

Habari hiyo, ambayo ilionekana Aisha alikuwa amelenga kuwafanya Watanzania waamini Ijumaa linaandika habari za ‘mezani’ alisema, yupo mwanaume mmoja aneyemsumbua kimapenzi kwa muda mrefu, ambaye ndiye aliyemfanyia unyambisi huo.
......mimi siyo Aisha niangalieni vizuri...!!!!!

“Huyo anayenichafua alikuwa ananitaka kimapenzi nikamkatalia na siwezi kumkubalia, hata kwa mtutu simpi mwili wangu ng’o, kuamua kunitangazia sifa chafu si suluhisho la mimi kumkubali, zaidi ya kumuona kichekesho kwani katika jamii ya watu wastaarabu hafai, namfananisha na ‘nungayembe’ la kiume,” alisema Aisha katika sehemu ya habari hiyo.

Aidha, aliongeza: “Picha za ngono zilizoenea kila kona ya nchi, zinazonihusu mimi si za kweli, amefanya hivyo kwasababu ‘nilimpiga za uso kavukavu bila chenga’, siwezi kupoteza muda wangu kubishana naye, nitakuwa nampandisha chati, lakini ajue hata kwa mtutu hapati kitu kwangu.” 

Katika juhudi za kulishusha ‘grade’ gazeti hili, sehemu ya habari hiyo ilisomeka, ‘Anadai amekuwa akikabiliwa na tuhuma za kupiga picha za ngono na utupu zilizosambazwa sehemu mbalimbali hasa katika magazeti ya udaku, ambapo kiuhalisia si zake.
....baada ya mitungi, mikasi....Aisha akiwa na Khumalo
Katika hatua nyingine, mapema wiki hii, kijana Khumalo aliyefanya naye uchafu huo nchini Afrika Kusini, amelitumia waraka pepe (e-mail) gazeti hili akiomba msahama kwa Aisha.

Alisema anakiri kumtenda vibaya (kupiga na kulikisha picha hizo) mnenguaji huyo, lakini anamuomba amsamehe na waanze ukurasa mpya