Thursday, November 21, 2013

Majeruhi Francis Shumira aliyepigwa risasi juzi na Gabriel Munis ili kulipiza kisasi kwa penzi la Christina afariki dunia



MAJERUHI Francis Shumira aliyejeruhiwa katika tukio la kushambuliwa kwa risasi Ilala Dar es salaam juzi  amefariki dunia jana asubuhi Hospitali ya Muhimbili alikolazwa MOI kwa matibabu. 
 
Kufariki kwa Francis kunafanya idadi ya watu  watatu waliofariki katika tukio hilo hadi hivi sasa huku ikiacha majeruhi wawili ambao  ni Christina Alfred Newa Mwanafunzi wa masuala ya Mawasiliano visiwa vya Syprus na mama mzazi wa Christina, Hellen Elieza Newa.

Familia imekiri kuwa Christina na Marehemu Munisi walikuwa na mahusiano lakini ni zamani na walitengana kutokana na vurugu alizowahi mfanyia siku za nyuma. 
Taarifa za Polisi zinapasha kuwa, Watu walio poteza maisha katika tukio hilo ni Gabriel  Munisi  ambaye aliwapiga  risasi  wenzake  na  kisha  kujiua  mwenyewe ,  Alfa Alfred ambaye  ni  mdogo wake Christina , na  Francis Khiranga Shumira ambaye  amefariki  jana  akiwa Muhimbili