Thursday, August 15, 2013

WANANCHI WAPEWA TAHADHARI KUHUSU NOTI BANDIA



BENKI Kuu ya Tanzania(BoT)Kanda ya Kaskazini Arusha imewatahadharisha wananchi kuchukua hatua mapema juu ya wimbi la noti bandia hapa nchini kwakuwataka wawemakini wakati wakutoa ama kupokea noti mpya ili kuepuka kufilisika na taifa kuyumba kiuchumi,anaripoti Richard Konga, Arusha.


Aidha benki hiyo imeanzisha utaratibu wakutoa elimu kwawananchi ili kutambua noti bandia na halali kupitia alama halisi zilizoko kwenye noti halali na kusisitiza kwa wananchi kuwa macho kwa kuzitambua alama hizo ilikuepuka kuruhusu matumizi ya noti feki kuingia kwenye mzunguko wa kawaida.

Akizungumza kwenye maonyesho ya wakulima Nanenane , Kandaya Kaskazini, Meneja wa Fedha na Utawala wa Benki hiyo,Eve na Ndesingo alisema kuwa BoT imeanza kutumia maonesho ya wakulima ya nanenane kutoa elimu ya utambuzi wa noti zake.

Alisema maonyesho yaliyofanyika jijini Arusha wananchi zaidi ya 10,000 wamepatiwa elimu ya utambuzi wa alama za noti mpya lengo ikiwa ni kuwafikia wananchi zaidi waliopo hapa nchini kupitia matawi yake.

Hata hivyo Ndesingo alibainisha kuwa matumizi ya noti bandia kwa jamii yamekuwa yakipungua mwaka hadi mwaka kutokana na jamii kuwa na uelewa wa noti halisi na bandia na hivyo kupunguza kasi ya mzunguko wa noti bandia kwa kiasi kikubwa.

Aidha alisema kuwa BoT kupitia matawi yake hapa nchini imejizatiti kuwa elimisha wananchi juu ya utambuzi wa noti mpya na alama zake ili jamiii zielewe na kutofautisha noti halali na bandia.

Alisema noti bandia iwapo zitaachwa ziendelee kuwepo kwenye mzunguko wamatumizi ya kawaida ipo hatari kwa jamii kufilisika sanjari na taifa kupoteza uchumi wake, kwahiyo aliitaka jamii kuwa makini sana pindi wanapokuwa wanapokea ama kutoa noti mpya kwa kuangalia alama zake halisi zikiwemo zakificho .

Akizungumzia namna ya kutambua noti halali za shilingi500, 2,000,5,000 na10 ,000,alisema zina alama ya kificho ambayo unaweza kuitambua kwakuipapasa kuangalia kwenye mwanga na kwamba alama hizo kwenye noti bandia hazipo na wala noti hizo hazina ubora unaotakiwa .

Ndesingo aliitahadharisha jamii kuwa makini pale inapofanya malipo ya noti mpya kwa kuchunguza kwamakini alama hizo kabla ya haijapelekwa kwa mtu mwingine.