Jeshi la
polisi nchini limeshaweka ulinzi wa kutosha katika msikiti wa Mtambani,
Kinondoni jijini Dar es Salaam kufuatia choko choko za maandamano
zilizopangwa kufanyika baada ya sara ya Ijumaa.
Kwa
mujibu wa kamera ya E.S.L Blog iliyoweka kambi eneo la tukio, mpaka
sasa gari tatu za polisi zimeshawasili eneo la msikiti huo kuimarisha
ulinzi.
"Ndugu
zangu msiogope kuja kusali leo ni jihadi, udhalilishaji wa serikali ya
CCM... LEO NI JIHADI. Msiogope kujakusali maana tumeshavipigia vyombo
vyote vya habari wakiwemo TBC 1, Channel 10, ITV na waandishinwote
watakuwepo kuona hichi walichopanga kukifanya hawa. Hayo ni maneno
ambayo yanatangazwa kwa sasa na kiongozi mmoja wa msikiti huu.
Mara
baada ya maneno haya naona magari ya askari yaliyokuwa yamepaki kwenye
mlango wa msikiti huo yameomdoka na kupaki pembezoni.
Ila mpaka
sasa hali ya usalama ni nzuri japo kumekuwa na choko choko za kufanyika
maadamano jambo ambalo linatia hofu wakati wa maeneo haya ambao
wameanza kufunga maduka yao.