Yadai
Ofisa wa Polisi anayeonekana kwenye picha, alikuwa akiwaelekeza watu
wasogee pembeni kwanza, akimwambia Slaa asubiri kidogo watengeneze njia
'vizuri' apite!
Tangu
mapema sana asubuhi, tumepokea simu kutoka maeneo mbalimbali ya nchi,
watu tofauti, wakionesha concerns zao juu ya taarifa kuwa ofisa mmoja wa
Jeshi la Polisi ameonekana kwenye picha 'akimdhibiti' Katibu Mkuu wa
CHADEMA, Dkt. Willbroad Slaa.
Picha na maelezo yake (caption) yameonekana kuwasononesha na kuwatisha watu wengi.
Ili
kusaidia jamii na kuepusha madhara makubwa yanayoweza kutokea, iwapo
usahihi wa tukio hilo hautaelezwa, tumeona ni vyema kwa nafasi yetu
kuweka kumbukumbu sawa.
USAHIHI; Kama ilivyo ada ya misafara ya
CHADEMA, hasa inapohusisha viongozi wakuu, viongozi (watendaji
waandamizi) wengine wa kitaifa, wabunge na viongozi wengine wa chama
katika maeneo husika, huwa ina hamasa, shamrashamra na mapokezi makubwa
kila mahali kunapofanyika mikutano au shughuli ya kichama.
Katibu
Mkuu, Dkt. Slaa na timu yake walipotua Mpwapwa kwa helkopta siku ya
Agosti 18, mwaka huu, alilakiwa na umati mkubwa wa watu, wakitaka
kumsalimia na kumkumbatia. Wakifurahia ujio wa mmoja wa viongozi wakuu
wa chama katika eneo lao, kwa ajili ya kuendesha Mabaraza Huru ya Rasimu
ya Katiba Mpya, katike eneo hilo.
Katika hali kama hiyo,
walinzi, wakiwemo askari polisi, walikuwa 'concerned' na hali ya
usalama, maana 'lolote' laweza kutokea. Ofisa wa Polisi anayeonekana
kwenye picha, alikuwa akiwaelekeza watu wasogee pembeni kwanza,
akimwambia Daktari asubiri kidogo watengeneze njia 'vizuri' apite, maana
watu wote wale kumfuata na kumkumbatia ingeweza kuwa hatari.
Kama
anavyoonekana, Dkt. Slaa naye alikuwa akijaribu kumwambia yule askari
kuwa awasaidie wale watu bila kuharibu utaratibu wa yeye kusalimiana na
wananchi wake, ambao hujaa kumlaki kwa nia njema, bila kukodiwa wala
kusombwa.
Hivyo ndivyo ilivyokuwa. Hakukuwa na 'kudhibitiana', bali kulikuwa na kuongozana.
Timu
ya Katibu Mkuu, kama ilivyo kwa Mwenyekiti Freeman Mbowe, kwa kutumia
usafiri wa chopa, inaendelea na ratiba ya kuendesha Mabaraza Huru ya
Rasimu ya Katiba Mpya, ambapo muda huu timu ya Mwenyekiti imeshaingia
Mkoa wa Katavi, kutokea Tabora na timu ya Dkt. Slaa iko Morogoro!
Maelfu
ya Watanzania wanaendelea kupata fursa ya kushiriki moja kwa moja,
kutoa maoni yao kwenye mabaraza hayo, yanayoendeshwa kwa njia ya wazi
kwenye mikutano ya hadhara.
Nawe unaweza kuendelea kutoa maoni
yako ya katiba, kwenye Mabaraza Huru ya Rasimu ya Katiba Mpya, kupitia
ujumbe mfupi kwenye namba 0789 248224 au email; chademamaoni@gmail.com