Thursday, August 15, 2013

BREAKING NEWZZZ: NYUMBA ZACHOMWA MOTO PWANI


Picha na Maktaba
Nyumba 6 zimechomwa moto katika Kijiji cha VODA ,Tarafa ya Mbwewe Mkoani Pwani,baada ya wanakijiji kuvamia gari la mizigo lililokuwa limebeba mitumba kuanguka na kufunga barabara ambapo wakazi hao walianza kupora hali iliyosababisha wenye mizigo kuingia kijijini kuwasaka waliopora mizigo hiyo.
Kamanda wa usalama barabarani Chalinze Afande Sule amesema sehemu ya barabara hiyo ya Chalinze-Segera imefungwa na kusababisha abiria kutoka Dar Es Salaam kwenda tanga,Kilimanjaro na Arusha kukwama.Chanzo itv