Sunday, August 11, 2013

CHAKULA CHAUA NDUGU WANNE,13 WENGINE HOI...



WATU wanne wa familia moja wamefariki na wengine 13
 wamelazwa hospitalini kutokana na kula chakula chenye sumu 

wakati wa sikukuu ya Idi el Fitri.Watu hao wamelazwa
 Kituo cha Afya cha Lusewa wilayani Namtumbo na Hospitali ya
Serikali ya Mkoa wa Ruvuma (HOMSO).


Kamanda wa Polisi Mkoa Deusidebit Nsimeki, alisema tukio hilo
 lilitokea Agosti 9, mwaka huu saa 7:00. Kamanda Nsimeki,
alisema siku hiyo kabla ya tukio, Salum Mumba, alinunua samaki 
aliyepeleka nyumbani kwa ajili ya sikukuu ya Idi.Kamanda
 Nsimeki alisema katika tukio hilo Polisi wanamshikilia
 mtu mmoja ambaye hakutaka kumtaja jina ambaye atasaidia polisi
 kwenye upelelezi wake. 
 

Alisema baada ya kula chakula hicho, haikuchukua muda mrefu
 mtoto alianza kuumwa naye baadaye alifariki dunia. Baadaye
watoto wawili walianza kuumwa na kufariki. Watu wengine 13
 walianza kuumwa baadaye majirani walipata taarifa kuwakimbiza
 watu hao hospitali. 
 

Aliwataja waliolazwa katika kituo cha afya cha Lusewa kuwa ni 
Tazamio Mumba, Zidani Mumba, Ramadhani Mumba na Zahara 
Mumba wote wakazi wa kitongoji Tulieni B. 
 

Waliolazwa katika hospitali ya Mkoa wa Songea kuwa ni Gairi
Mumba, Zamoni Mumba, Fatuma Rashidi, Samidu Mumba, Asha
 Omary na Sharifa Mumba. 

Kwa upande wake Mganga Mfawidhi ya Hospitali ya Mkoa Songea Dkt. Benedictor Ngaiza alisema wagonjwa waliolazwa hospitalini hapo hali zao zinaendelea vizuri.